IQNA

Ujumbe wa wasomaji Qur'ani Wairani waelekea Makka

11:53 - November 04, 2010
Habari ID: 2025346
Ujumbe wa wasomaji Qur'ani wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran umeondoka Tehran Jumatano hii ukielekea katika miji mitakatifu ya Makka na Madina.
Kwa mujibu wa IQNA, wanachama wote 32 wa ujumbe huo wanatazamiwa kukutana mjini Makka siku ya Ijumaa.
Ujumbe huo uliopewa jina la Nur unajumuisha wasomaji mahiri zaidi na maqari bora zaidi wa Qur'ani Tukufu nchini Iran. Aidha ujumbe huo unajumuisha kundi moja la Qaswida.
Kwa kawaida mahujaji huvutiwa sana na visomo vya maqari Wairani ambao hushiriki katika ibada ya hija kila mwaka.
688013
captcha