IQNA

Iran na Cyprus kushirikiana katika sekta za utamaduni, elimu

10:27 - November 07, 2010
Habari ID: 2026467
Waziri wa Utamaduni na Miongozo ya Kiislamu wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran Dkt. Sayyid Muhammad Husseini amekutana na kufanya mazungumzo na Andreas Demetriou Waziri wa Elimu na Utamaduni wa Jamhuri ya Cyprus.
Katika mkutano huo uliofanyika mjini Tehran mawaziri hao wawili wamejadili njia za kuimarisha uhusiano. Aidha Wizara ya Utamaduni na Elimu ya Cyprus imetiliana saini makubaliano ya ushirikiano na Wizara ya Elimu ya Iran.
Cyprus ni nchi iliyo mashariki mwa Bahari ya Mediterranean kusini mwa Uturuki na magharibi mwa Syria na Lebanon.
Cyprus ni mwanachama mwanzilishi wa Jumuiya ya Nchi Zisizofungamana na Siasa za Upande Wowote na ilijiunga na Umoja wa Ulaya Mei Mosi 2004. Takribani asilimia 78 ya wakaazi wa nchi hiyo ni Wakristo na asilimia 18 ni Waislamu.
689592
captcha