Sambamba na kufanyika ibada ya hija katika jangwa la Arafa katika mji mtakatifu wa Makka katika siku ya Arafa tarehe 9 Dhul Hijja, Waislamu wa Ufaransa watajiunga na wenzao duniani kote katika hafla ya kimaanawi ya kusoma Dua ya Arafa itafanyika siku hiyo mjini Paris katika ukumbi wa Baitul Zahra (AS).
Kwa mujibu wa tovuti ya beytolzahra, hafla hiyo iliyoandaliwa na Jumuiya ya Baitul Zahra (AS) itawakutanisha pamoja Waislamu wa matabaka mbalimbali wakiwemo Wairani wanaoishi mjini Paris.
Mbali na kusomwa dua ya Arafa, hafla hiyo pia itajumuisha kisomo cha Qurani Tukufu, Sala ya Jamaa na hotuba za Maulamaa.
Jumuiya ya Baitul Zahra (AS) pia imewatangazia Waislamu wa Paris kuwa Dua Kumayl husomwa kila Alhamisi saa moja usiku katika ukumbi wa jumuiya hiyo.
689589