IQNA

Kikao cha kimataifa cha "Halali" kufanyika nchini Uingereza

16:48 - November 09, 2010
Habari ID: 2028881
Kikao cha kimataifa cha Halal kimepangwa kufanyika tarehe 19 na 20 mwezi huu wa Novemba mjini London Uingereza. Kikao hicho kitajadili na kuchunguza sekta ya viwanda na biashara ya nyama halali.
Taarifa iliyotolewa na Baraza la Kiislamu la Uingereza imesema kuwa kikao hicho kitachunguza mustakbali wa sekta na biashara ya nyama halali nchini humo na barani Ulaya na matatizo na changamoto zinazowakabili wazalishaji nyama halali.
Kikao hicho kitajadili masuala mbalimba kama suala la kustawishwa viwanda na biashara ya nyama halali, kushughulikia masuala ya watumiaji katika nchi za Magharibi, bidhaa za halali mahotelini na suala la kuanzishwa jumuiya rasmi za bidhaa halali katika nchi za Uingereza na Norway.
Kikao hicho kitasimamiwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Halali (IHI) ikishirikiana na Idara ya Viwanda na Biashara ya Kiislamu ya Malaysia (ICCI) na wazalishaji wa bidhaa za halali. 692096
captcha