IQNA

Kongamano la Kimataifa la Hija laanza Makka

18:57 - November 10, 2010
Habari ID: 2029667
Kongamano la Kimataifa la Hija chini ya anuani ya, 'Ufahamu wa Kiislamu katika Siku za Hija' limeanza leo Novemba 10 katika mji mtakatifu wa Makka.
Kwa mujibu wa tovuti ya hajinformation kongamano hilo linafanyika kwa himaya ya Wizara ya Hija ya Saudi Arabia kwa lengo kuongeza maarifa na kubadilishana mawazo kuhusu mitazamo mbalimbali ya hija na masuala husika. Aidha kongamano hilo linakusudia kutathmini njia za kuwahudumia mahujaji ili kuwawezesha watekeleze amali za hija kwa njia sahali bila matatizo.
Kongamano hilo la kimataifa limefunguliwa na Waziri wa Hija wa Saudi Arabia Fuad bin Abdulsalam al Farisi na kuhudhuriwa na maulamaa kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu.
692823
captcha