Kwa mujibu wa Mwambata wa Utamaduni wa Iran mjini Nairobi, kongamano hilo litawashirikisha wasomi na watafiti ambao watajadili masuala kama vile, 'Qur'ani: Masuala ya Kimaadili kuhusu Sayansi ya Kisasa, Qur'ani na Botania, Qur'ani na Afya, Qur'ani na Embriolojia, Qur'an na Sayansi za Kisasa, Qur'ani na Anga za Mbali, Qur'ani na Uadilifu wa Kiuchumi, Qur'an na Masuala ya Mazingira, Qur'ani na Changamoto Zinazomkabili Mwanadamu Duniani, Qur'ani: Masuala ya Kifilosofia na Kianthropolojia na Qur'ani na Masuala ya Dini Mbalimbali.
Kongamano hilo litafanyika kuanzia Machi 10-12 mwaka 2011 katika Chuo Kikuu cha Nairobi, Kenya.
Wanaotaka kushiriki katika kongamano hilo wanatakiwa kuwasilisha mukhtasari wa makala zao kufikia Februari 15, 2011.
Kwa maelezo zaidi wasiliana na Idara ya Utamaduni ya Jamburi ya Kiislamu ya Iran, SLP 59595-00200 Nairobi-Kenya
Simu +245 20 2214352 +254 20 318833
Barua pepe: iranlib@yahoo.com
694264