IQNA

Treni ya kasi yazinduliwa Makka

12:00 - November 14, 2010
Habari ID: 2031272
Awamu ya kwaniza ya treni ya kasi ya mji Mtakatifu wa Makka imezinduliwa Novemba 13 asubuhi kwa lengo la kupunguza msongamano wa mahujaji katika msimu wa Hija.
Reli ya kilomita 18 ambayo katika awamu ya kwanza ina vituo tisa itaunganisha mji wa Makka na maeneo matakatifu ya ibada ya hija ya Mina, Arafat na Muzdalifa na ina uwezo wa kubeba abiria 72 lefu kwa saa.
Mradi huo wa reli ambayo pia inajulikana kama Reli ya Mashair umetekelezwa kwa ushirikiano wa China na Saudi Arabia na unatazamiwa kukamilika Mei 2011. Mradi huo umegharimu dola bilioni 1.8.
Mabasi 4000 yalikuwa yakitumika kuwasafirisha mahujaji katika masafa ya reli hiyo.
694208
captcha