IQNA

Kuhudumia Qur'ani ni fakhari

11:47 - November 16, 2010
Habari ID: 2032819
Mkuu wa Masuala ya Utamaduni katika Shirika la Utamaduni na Uhusiano wa Kiislamu amesema kuihudumia Qur'ani ni fahari ya shirika hilo.
Mohsen Pakayin ameyasema hayo mjini Tehran Jumatatu 15 Novemba katika sherehe za kuanzishwa vitengo vya lugha za Myanmar na Kazakh katika Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa IQNA.
Ameongeza kuwa ni fakhari kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kuwa shirika la kwanza la habari za Qur'ani duniani liko katika nchi ya Kishia.
Amesema katika dunia ya leo, kuarifisha Qur'ani kwa walimwengu na kueneza mafundisho yake ni masuala muhimu mno ili kukabiliana na chuki dhidi ya Uislamu na hujuma ya kipropaganda ya maadui.
Kwa kuongezwa lugha hizo mbili, idadi ya lugha katika Shirika la Habari za Qur'ani la Kimataifa imefika 31.
696172



captcha