IQNA

Mashindano ya Qur'ani ya Jeshi la Iran

14:37 - November 21, 2010
Habari ID: 2034397
Fainali ya Mashindano ya Qur'ani ya vikosi vya nchi kavu vya Jeshi la Jamhuri ya Kiislamu ya Iran itafanyika Jumapili Novemba 21 katika mji wa Isfahan kati wa Iran.
Baada ya mashindano ya mchujo, washiriki watachuana kitaifa katika viwango vya Qiraa ya Qur'ani, kuhifadhi Qur'ani, Tafsiri, Ufahamu wa Qur'ani, Hadithi na Adhana.
Watakaoshinda watafuzu kuingia katika mashindano ya Qur'ani ya vikosi vyote vya kijeshi vya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran yatakayofanyika Disemba mwaka huu.
697059
captcha