IQNA

Mashindano ya Kitaifa ya Kuhifadhi Qur'ani yaanza Imarati

14:22 - November 28, 2010
Habari ID: 2038781
Duru ya Saba ya Mashindano ya Kitaifa ya Kuhifadhi Qur'ani yanaaza alasiri leo Novemba 28.
Kwa mujibu wa gazeti la Al Khalij mashindano hayo yanasimamiwa na Taasisi ya Kimataifa ya Zawadi ya Dubai na yatajumuisha wanawake na wanaume.
Mkuu wa Kamati ya Uandalizi Ibrahim Muhammad Bumilha amesema mashindano haya yatamalizika Novemba 29. Amesema jopo la majaji katika mashindano hayo litajumuisha wataalamu 18 wanaume na wanawake.
Ahmad Safar al Sayvidi mwanachama wa Kamati ya Maandalizi amesema washindi watatunukiwa zawadi katika hafla maalumu.
702468
captcha