IQNA

Mashirika 21 ya kimataifa yataka kuondolewa mzingiro wa Gaza

13:02 - December 01, 2010
Habari ID: 2040716
Mashirika 21 ya kimataifa ya kutetea haki za binadamu yametaka kutafutwa ufumbuzi mpya wa kumaliza haraka iwezekanavyo mzingiro unaotekelezwa na utawala haramu wa Israel dhidi ya wakazi wasio na hatia wa Ukanda wa Gaza.
Kwa mujibu wa tovuti ya Palestine info, mashirika hayo yalitoa taarifa hapo jana Jumanne yakisisitiza kwamba ulegezaji utawala huo mzingiro huo haujakuwa na athari yoyote katika kupunguza machungu na matatizo ya kimaisha ya wakazi wa Ukanda wa Gaza.
Mashirika hayo ambayo yanajumuisha pia Shirika la Msamaha Duniani Amnesty International na Shirika la Norway la Kutetea Wakimbizi yametangaza kwamba utawala haramu wa Israel pia unazuia kuingizwa katika Ukanda wa Gaza bidhaa muhimu za ujenzi.
Yamesema ulegezwaji wa mzingiro wa Gaza umesaidia tu katika kurahisisha utembeaji wa raia wa Gaza lakini kwamba ungali unazuia kuingizwa katika ukanda huo bidhaa muhimu za misaada ya kibinadamu. 704653
captcha