Hayo ni kwa mujibu wa Badrudin Abdul Hakim Al Warfawi, mwakilishi wa Libya katika Mashindano ya Tatu ya Kimataifa ya Qurani kwa Ajili ya Wanachuo Waislamu. Qari huyo wa Misri amesema kuwa mashindano kama hayo ya Qurani vile vile yana mchango mkubwa katika kuimarisha uhusiano miongoni mwa nchi za Kiislamu.
Akizungumza na IQNA amesema kuwa: “Nimeshiriki katika mashindano ya Qurani nchini Libya na kushinda zawadi kadhaa. Baada ya kuibuka mshindi katika mashindano yaliyopita, nimeamua kushiriki katika mashindano ya kimataifa nchini Iran”
Al Warfawi ameashiria harakati za Qurani nchini Libya na kusema: “Kila mwaka Libya huandaa mashindano ya kimataifa ya Qurani ambayo huwa na washiriki kutoka nchi za Kiislamu ikiwemo Jamhuri ya Kiislamu ya Iran”.
704405