IQNA

Kumbukumbu ya kuuawa shahidi Imam Hussein kuonyeshwa katika televisheni ya Uturuki

9:52 - December 02, 2010
Habari ID: 2040933
Kipindi cha shughuli za mwezi wa Muharram za kukumbuka mauaji ya mjukuu wa Mtume Muhammad (saw) Imam Hussein bin Ali (as) na masahaba zake katika uwanja wa Karbala kitaonyeshwa katika televisheni ya taifa ya Uturuki (TRT) sambamba na kuanza mwezi mtukufu wa Muharram.
Kipindi hicho cha televisheni kinaonyeshwa kwa shabaha ya kuarifisha tukio la Ashuraa na kuuawa shahidi Imam Hussein (as) na masahaba zake.
Mpango wa televisheni ya serikali ya Uturuki ya TRT wa kuarifisha tukio la Ahuraa ulianza mwaka 2007 kwa kuonyesha kipindi maalumu kuhusu matukio ya Karbala kilichopewa jina la 'Mahala Pote ni Karbala'. Vipindi hicho mbali na kuarifisha Ahlul Bait wa Mtume Muhammad (saw), vinabainisha sababu za uadui wa Bani Umayyah dhidi ya Imam Ali bin Abi Twalib (as), sababu za suluhu na mapatano ya Imam Hassan (as) na Muawiyah bin Abi Sufian, mapambano ya Imam Hussein (as) huko Karbala, itikadi ya Imam wa Zama (as) na umuhimu wa tukio la Ashuraa. 704601

captcha