IQNA

Mashindano ya kitamataifa ya Qur'ani ya Sayyid Juneid yaanza nchini Bahrain

16:58 - December 07, 2010
Habari ID: 2043974
Duru ya nane ya mashindano ya kimataifa ya Qur'ani Tukufu yanayofanyika chini ya anwani ya Sayyid Juneid imeanza katika Kituo cha Kiislamu cha Ahmad al-Fatih katika mji wa Manama nchini Bahrain.
Gazeti la nchi hiyo la al-Watan limeandika kwamba mashindano hayo yameandaliwa na Jumuiya ya Huduma za Qur'ani ya Bahrain. Licha ya kuhifadhi Qur'ani mashindano hayo pia yatahusu nyanja nyinginezo zinazohusiana na kitabu hicho kitakatifu.
Mashindano hayo yatamalizika hii leo Jumanne na sherehe ya kuyafunga kufanyika hapo kesho Jumatano badaa ya kuswaliwa swala za Maghrib na Ishaa. Wawakilishi kutoka nchi za Bahrain, Kuwait, Imarati, Saudi Arabia, Libya, Bangladesh, Oman, Ugiriki, Morocco, Tajikistan, Qatar, Sudan, Chad, Iraq, Yemen, Jordan, Syria, Palestina, Lebanon na Pakistan wanashiriki katika mashindano hayo. 708092
captcha