IQNA

Morocco yatoa msaada wa dirhamu milioni moja kwa ajili ya kutetea Quds Tukufu

17:17 - December 11, 2010
Habari ID: 2046063
Baraza la mji wa Fas nchini Morocco limetoa msaada wa dirhamu milioni moja kwa ajili ya kutetea turathi za kiutamaduni na ustaarabu wa Kiislamu katika mji mtakatifu wa Quds huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu.
Mwenyekiti wa baraza la mji huo Hamid Shabab amesema kuwa fedha hizo zitatumika kwa ajili ya kutoa sura mpya ya mpango wa miji dada ya Fas na Quds na vilevile kutekeleza ratiba mbalimbali za kupanua na kustawisha utamaduni wa Quds Tukufu.
Vilevile amepongeza juhudi za Mfalme Muhammad wa Sita wa Morocco za kulinda historia, utamaduni na ustaarabu wa Kiislamu wa mji wa Quds huko Palestina na kukabiliana na njama za kutaka kuuyahudisha mji huo wa Kiislamu. 710296

captcha