IQNA

Vitivo vya Sayansi za Qur'ani Iran vyasajili wanachuo wa Ph.D

14:16 - December 20, 2010
Habari ID: 2050356
Vitivo vya Sayansi za Qur'ani katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran vimepanga kusajili wanachuo wapya wa shahada ya uzamivu (Ph.D) katika mustakabali wa karibu, amesema Mkuu Chuo Kikuu cha Awqaf cha Sayansi za Qur'ani na Utamaduni.
Kwa mujibu wa idara ya habari ya uhusiano wa kimataifa katika Shirika la Awqaf, Hujjatul Islam Muhammad Ali Raghebi amesema kuna vitivo 14 vya sayansi za Qur'ani nchini Iran ambapo kuna wanachuo 3000 katika shahada ya kwanza (BA) na shahada ya uzamili (M.A).
"Watakaofuzu katika shahada ya uzamivu watajiunga na mabaraza ya kisayansi ya vitivo hivyo", ameongeza Sheikh Ali Raghebi.
Aidha amesema kuwa nchini Iran athari za Qur'ani zinabainika katika mazungumzo na tabia za wananchi. Vilevile amesema washindi wa mashindano ya Qur'ani wanaweza kusajiliwa katika vitivo vya sayansi za Qur'ani bila kufanya mitihani.
714601
captcha