Duru ya saba ya mashindano ya kimataifa ya usomaji Qur'ani Tukufu, ambapo wawakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran wanashiriki, yataanza hapo kesho Jumatano katika mji wa Bhopal huko India.
Tovuti ya Ummid imeripoti kuwa wasomaji wa Qur'ani Tukufu kutoka India na nchi nyingine za dunia zikiwemo Iran, Pakistan, Uingereza na Panama watashiriki katika mashindano hayo.
Mashindano hayo ambayo yameandaliwa na Jumuiya ya Kimataifa ya Zinat al-Qur'an yataendelea kwa muda wa siku mbili. Washindi wa kwanza hadi nne watatunukiwa zawadi nono ya fedha na washiriki wengine wote kuzawadiwa loho ya shukrani na ukumbusho. 715813