Kwa mujibu wa tovuti ya Chuo Kikuu cha Menejmenti na Teknolojia cha Lahore UMT, kongamano hilo litafanyika kwa usimamizi wa kitivo cha Sayansi za Jamii chuoni UMT kuanzia 9-10 Machi.
Kati ya masuala yatakayojadiliwa ni pamoja na 'nafasi na ustawi wa ustaarbu wa Kiisamu, 'sifa za ustaarabu wa Kiislamu na athari zake kwa staarabu zingine kubwa duniani', 'umoja wa anuai katika ustaarabu wa Kiislamu', 'nafasi ya ustaarabu wa Kiislamu katika fikra za kidini, sayansi za kijamii na kimaumbile na uhusiano wa kimataifa, sanaa, utamaduni, usanifu majengo na sheria'.
Makala katika kongamano hilo zitakuwa kwa lugha Kiingereza na Kiarabu. 716789