IQNA

Ripoti mpya ya mzingiro haramu wa Ukanda wa Gaza

12:37 - December 25, 2010
Habari ID: 2052653
Kituo cha Haki za Binadamu cha Palestina kimetoa ripoti mpya kuhusiana na kuendelea mzingiro usio wa kisheria unaotekelezwa na utawala haramu wa Israel katika Ukanda wa Gaza.
Ripoti hiyo inabainisha kwa kina baadhi ya athari mbaya za mzingiro huo dhidi ya wakazi madhlumu wa Ukanda wa Gaza na kuendelea upuuzaji wa utawala wa Kizayuni dhidi ya matakwa ya walimwengu kuhusiana na udharura wa kuondolewa mzingiro huo.
Uvamizi wa Wazayuni katika Ukanda wa Gaza ulimalizika mwaka 2004 lakini tokea wakati huo hadi sasa ukanda huo umekuwa chini ya mzingiro mkubwa wa utawala haramu wa Israel.
Mzingiro huo ulizidishwa mwaka 2007 ambapo mawasiliano ya karibu watu milioni 1.7 wanaoshi katika ukanda huo na ulimwengu wa nje yamekatwa kikamilifu. 717398
captcha