IQNA

Ombi la kugawa Qur'ani katika shule za mji wa Waterloo

11:42 - January 02, 2011
Habari ID: 2056891
Kituo cha Habari cha Kiislamu cha Chuo Kikuu cha Waterloo kimepiga hatua mpya ya kutoa ombi la kugawa nakala moja ya Qur'ani Tukufu kwa kila mwanafunzi wa darasa la tano la shule za Waterloo katika mkoa wa Ontario nchini Canada.
Kituo cha Habari cha The Record kimeripoti kuwa mbali na kutoa ombi hilo kwa Jumuiya ya Shule za eneo hilo, Kituo cha Habari cha Kiislamu cha Waterloo kimetangaza kuwa iwapo ombi hilo litakubaliwa kitatoa nakala ya Qur'ani Tukufu kwa kila mwanafunzi wa darasa la tano katika mwaka wa masomo wa 2011-2012.
Hatua hiyo imechukuliwa kwa lengo la kuwaelimisha wanafunzi na familia zao kitabu kitakatifu cha Qur'ani kupitia tarjumi ya Kiingereza ya kitabu hicho cha Mwenyezi Mungu. 722211
captcha