Ibrahim Alkad amewataka Waislamu wa Ghana kujiepusha na husuda, kiburi, chuki na mambo mengine yanayokwenda kinyume na maadili mema ya kijamii.
Sheikh Ibhahim Alkad ameliambia shirika la habari la Ghana katika mji wa Kumasi kwamba: "Sisi Waislamu tunalazimika kuwa kigezo bora cha maisha mema kwa watu wa jamii."
Amesema Waislamu na wafuasi wa dini nyingine wanapaswa kumuomba Mwenyezi Mungu ili awasamehe dhambi zao na kuwaangalia kwa jicho la huruma. 728831