IQNA

Iran yaizawadia Brunei nuskha za Qur'ani

11:29 - January 13, 2011
Habari ID: 2063860
Ubalozi wa Jamhuri ya Kiislamu nchini Brunei umeizawadia shule ya sekondari ya Sayyidna Hussein (as) nuskha kadhaa za Qur'ani Tukufu.
Kwa mujibu wa tovuti ya BruDirect nuskha hizo zimeandamana na tarjumi za Kiingereza na Kifarsi za aya za Qur'ani.
Haji Jaafari bin Haji Suheili, mkuu wa shule hiyo amepokea nuskha hizo kutoka kwa Muhammad Ashtiyani, Balozi wa Iran nchini Brunei. Balozi Ashtiyani ametangaza kuwa ubalozi huo una mpango wa kusambaza nuskha zaidi za Qur'ani katika shule zote za Brunei.
Amesema tarjumi hizo za Qur'ani zimechunguzwa na kupitishwa na taasisi na vituo mbalimbali vinavyojushughulisha na masuala ya Qur'ani nchini Iran. 729221
captcha