IQNA

Vipawa vipya vyaibuka katika Mashindano ya Qur'ani ya wanachuo

13:08 - January 18, 2011
Habari ID: 2066420
Kuibuka vipawa vipya vya Qur'ani ni kati ya matokeo mazuri ya Mashindano ya Tatu ya Kimataifa ya Qur'ani ya Wanachuo yaliyofanyika hivi karibuni katika mji wa Mash'had kaskazini mashariki mwa Iran.
Abbas Salimi ambaye aliongoza jopo la majaji katika mashindano hayo amesema Mashindano ya Tatu ya Kimataifa ya Qur'ani ya Wanachuo yalikuwa fursa nzuri kwa vijana kuwafahamu wataalamu na wasomi wa Qur'ani Tukufu. Ameongeza kuwa aghalabu ya washiriki katika viwango vya qiraa na hifdhi walikuza vipawa vyao kwa kiwango kikubwa.
Ustadh Salimi amesema wanachama wote katika jopo la majaji walikuwa na uzoefu mkubwa na wanafahamika kimataifa. Amesema vitengo vingine kama vile utafiti kuhusu masuala ya Qur'ani vinaweza kuongezwa katika mashindano yajayo.
730973
captcha