IQNA

Mashindano ya Qur'ani kwa vijana wa Kuwait

13:11 - January 18, 2011
Habari ID: 2066569
Duru ya kwanza ya mashindano ya kitaifa ya utamaduni, elimu na jamii ya Kuwait yamepangwa kuanza hivi karibuni nchini humo kwa kufanyika mashindano ya Qur'ani na Tajwidi.
Kwa mujibu wa gazeti la nchi hiyo la al-Anbaa, mashindano hayo yanaandaliwa na Idara Kuu ya Vijana na Michezo ya Kuwait kwa ushirikiano wa Idara ya Masuala ya Qur'ani inayofungamana na Wizara ya Wakfu na Masuala ya Kiislamu. Mashindano hayo yamepangwa kufanyika katika makundi mawili ya vijana walio na umri wa miaka 10 hadi 16 na 17 hadi 29. Mshindi wa kwanza wa mashindano hayo atapewa zawaidi ya dinari 500 za Kuwait, wa pili dinari 400, wa tatu dinari 300, wa nne dinari 200 na wa tano dinari 150.
Idara Kuu ya Vijana na Michezo ya Kuwait imewataka vijana walio na hamu ya kushiriki kwenye mashindano hayo kusajili majina yao kupitia anwani ifuatayo ya mtandao: www.islam.gov/quran au kufika kwenye ofisi za idara hiyo katika eneo la ar-Raq'i. Muhula wa mwisho wa kusajili majina hayo ni tarehe tarehe 3 Februari.
Idara hiyo imetangaza kuwa lengo la mashindano hayo ni kuandaa mazingira ya mashindano kati ya vijana kuhusiana na masuala ya kidini na kiutamaduni. Imewataka vijana kushiriki kwa wingi katika mashindano hayo ili kunyanyua kiwango chao cha malezi bora ya nafsi. 731847
captcha