Kwa mujibu wa tovuti ya Noor, Profesa Harald Schneider amesilimu na kuamua kufuata madhehebu ya Shia wakati akifanya utafiti katika mji wa Karbala nchini Iraq.
Profesa Harald Schneider ametoa taarifa akisema: “Nilikuwa nimesafiri kwa mara ya pili katika mji mtakatifu wa Karbala. Mara hii nilipoingia katika Haram Takatifuya Imam Hussein , nilipata hisia nzuri ambayo siwezi kuifafanua kwa maneno, hisia ambayo nilikuwa sijawahi kuipata maishani”.
Harald Schneider amechagua jina la Kiislamu la Hassan na kuongeza kuwa, “itikadi za madhehebu ya Shia daima zinaenda sambamba na fikra zangu binafsi”.
Abdul Mahdi Karbalai, msimamizi wa Haram Takatifu ya Imam Hussein AS amemfahamisha profesa huyo Mjerumani historia fupi ya matukio ya kusikitisha ya Karbala na vilevile malengo ya harakati ya Imam Hussein AS.
733515