Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Uingereza amesema serikali ya London inapinga misimamo mikali na kwa sababu hiyo imekataa kutoa viza kwa Kasisi Terry Jones ambaye imesema amekuwa akitoa matamshi yanayoakisi mwenendo wake usiokubalika. Amesema kuwa Uingereza hairuhusu watu kama hao ambao hawahudumii maslahi ya taifa kuingia nchini humo.
Jumuiya ya watu wanaopinga wahajiri wa kigeni ilikuwa imemwalika Kasisi Terry Jones kutembelea Uingereza. Hata hivyo kundi linalopinga misimamo mikali limeitaka serikali ya London kumzuia kasisi huyo asiingie nchini humo kutokana na misimamo yake ya kibaguzi dhidi ya dini ya Kiislamu hususan Kitabu Kitakatifu cha Mwenyezi Mungu Qur'ani. 734630