IQNA

Kikao cha tatu cha mawaziri wa nchi za Kiislamu kufanyika Libya

10:34 - January 24, 2011
Habari ID: 2069085
Kikao cha tatu cha mawaziri na maafisa wa nchi za Kiislamu kimepangwa kufanyika tarehe 10 na 11 za mwezi Februari huko Tripoli mji mkuu wa Libya kwa lengo la kuchunguza masuala ya watoto.
Kikao hicho ambacho kimeandaliwa na Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Jumuiya ya Nchi za Kiislamu ISESCO kitachunguza juhudi za maendeleo na changamoto zinazowakabili watoto wa ulimwengu wa Kiislamu katika miaka yao ya kwanza maishani.
Sheria zinazowalinda watoto, utekelezaji wake na kuasisiwa kwa jumuiya ya watoto katika ulimwengu wa Kiislamu ni masuala mengine yatakayochunguzwa kwenye kikao hicho. 734520
captcha