IQNA

Maombolezo ya Mtume (saw) kufanyika New York

13:07 - January 31, 2011
Habari ID: 2073093
Maombolezo ya kukumbuka siku ya kuaga dunia Mtume Mtukufu Muhammad (saw) yamepangwa kufanyika kesho Jumanne katika Kituo cha Waislamu wa madhehebu ya Shia Ithna Asheri mjini New York Marekani SIJNY.
Kwa mujibu wa tovuti ya kituo hicho, maombolezo hayo yatakayoanza saa 12:30 kwa wakati wa New York yataendelea kwa muda wa masaa matatu.
Usomaji wa sura ya Yasin, dua ya Tawassul na ziara ya Mtume Muhammad (saw) ni miongoni mwa ratiba za maombolezo hayo ambayo yataendeshwa kwa lugha mbili za Kiingereza na Kiurdu. Kituo hicho cha Kiislamu pia kimeandaa maombolezo ya kukumbuka kifo cha mtukufu mwingine wa Kiislamu Imam Ali bin Mussa Ridha (as) ambaye ni mjukuu wa Mtume (saw) katika siku ya Jumatano. 739390
captcha