Sambamba na siku ya kwanza ya sherehe za Alfajiri Kumi za kuadhimisha Ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran na tukio la kurejea nchini hayati Imam Khomeini Mwenyezi Mungu amrehemu baada ya kuishi uhamishoni kwa kipindi cha miaka 15, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Ayatullah Ali Khamenei mapema Februari Mosi alizuru kaburi la muasisi wa Jamhuri ya Kiislamu Imam Khomeini MA na kumsomea al Fatiha.
Kaburi hilo liko kusini mwa Tehran.
Baadaye Ayatullah Khamenei amezuru makaburi ya mashahidi wa siku ya tarehe 7 Tir (kwa mwaka wa Kiirani) na mashahidi wengine wa Mapinduzi ya Kiislamu katika makaburi ya Behesht Zahra na kuwaombea dua na maghufira.
740258