IQNA

Kikao cha "Quds katika Fikra za Kiislamu" kufanyika Ufaransa

18:47 - February 05, 2011
Habari ID: 2075688
Kikao cha Quds katika Fikra za Kiislamu kimepangwa kufanyika tarehe 15 Februari katika mji wa Marseille nchini Ufaransa.
Tovuti ya Saphirnews imeripoti kuwa kikao hicho ambacho kitakuwa mkutano wa kwanza wa Waislamu wa Ufarasna katika mwaka huu wa 2011 kitasimamiwa na Muungano wa Familia za Kiislamu (UFM).
Miongoni mwa wageni wa kikao hicho ni Sheikh Ghalib bin Sheikh, mtaalamu wa masuala ya Kiislamu na Mwenyekiti wa kongamano la Kimataifa la Dini kwa Ajili ya Amani. 742232

captcha