IQNA

Masomo ya Qur'ani kufanyika Kadhimein

16:30 - February 06, 2011
Habari ID: 2076236
Taasisi ya Qur'ani ya mjini Kadhimein nchini Iraq imepanga kuandaa masomo ya kuvutia ya sheria za kiraa na tajwidi ya Qur'ani Tukufu.
Taasisi hiyo imetangaza kuwa masomo hayo pamoja na mbinu za wasomaji mashuhuri wa Qur'ani wa Iraq yataanza kufundishwa hivi karibuni katika mji huo.
Sayyid Hussein Ismail as-Swadr ambaye ni muasisi wa tasisi hiyo ya Qur'ani amesema kuwa masomo hayo yataendeshwa na wasomaji mashuhuri wa Qur'ani akiwemo Sheikh Mahmoud al-Karkhi.
Taarifa ya taasisi hiyo imesema kuwa watu watakaohitimu masomo hayo watapewa vyeti na vibali vya kusoma Qur'ani nchini Iraq na kwingineko. 742489
captcha