Kwa mujibu wa gazeti la as-Sharq linalochapishwa nchini Qatar kituo hicho kipya kimeanzishwa kwa madhumuni ya kuzidisha idadi ya wanafunzi walio na hamu ya kujifunza masomo ya Qur'ani na kuwashajiisha wanawake zaidi washiriki katika masomo hayo.
Kituo hicho ambacho kina suhula za kisasa za mafunzo kinatazamiwa kuimarisha zaidi shughuli za mafunzo ya Qur'ani nchini Qatar.
Vipindi zaidi vya masomo vimeongezwa katika ratiba ya masomo ili kuimarisha viwango vya masomo katika kituo hicho kipya. 742964