Gavana wa Bauchi Isa Yuguda amewataka wakuu wa mabaraza ya miji minne ya jimbo hilo kutoa maelezo ni kwa nini wakilishi wao hawakushiriki katika mashindano ya kusoma Qur'ani ya jimbo hilo.
Amesisitiza kuwa wakuu wa miji hiyo wanapaswa kutoa maelezo ni kwa nini wamewazuia vijana kushiriki katika mashindano hayo.
Gavana Isa Yuguda amezitaka pia familia za Kiislamu za Nigeria kuwatayarishia uwanja nzuri watoto wao kwa ajili ya kuhifadhi Qur'ani Tukufu.
Mashindano ya 25 ya kusoma Qur'ani ya jimbo la Bauchi yalifanyika tarehe 30 Januari yakiwashirikisha wasomaji 140. 743443