Kituo cha habari cha Uganda Media Center kimeripoti kuwa Rais Yoweri Museveni amewataka maulamaa wa Kiislamu wa Uganda kushirikiana na kuimarisha umoja wao. Amesisitiza kuwa umoja na mshikamano ni jambo la dharura kwa ajili ya amani na utulivu wa Uganda.
Kumekuwapo mivutano ya muda mrefu sasa kati ya makundi mawili ya Waislamu nchini Uganda, suala ambalo linatishia umoja wa wafuasi wa dini hiyo. 747727