IQNA

Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Qur'ani Iran ateuliwa

16:25 - February 15, 2011
Habari ID: 2081022
Hassan Muhammadi ameteuliwa kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Jumuiya ya Taasisi za Qur'ani katika Jamhuri ya Kiislamu ya Iran.
Kwa mujibu wa mwandishi wa IQNA, katika kikao kilichofanyika wiki iliyopita Muhammadi aliteuliwa katika mkutano uliojumuisha taasisi zote za Qur'ani nchini Iran. Hassan Muhammadi ana shahada ya uzamili katika sayansi za Kiislamu na usimamizi wa Kifedha kutoka Chuo Kikuu cha Imam Sadeq AS cha Tehran.
Muhammadi amekuwa akifanya kazi kwa muda wa miaka mitano katika Jumuiya ya Taasisi za Qur'ani ya Iran kama mkurugenzi wa masuala ya utendaji na fedha.
Muhammadi anachukua nafasi ya Reza Mokhtari.
747595
captcha