IQNA

Mashindano ya Qur'ani yafanyika kitaifa India

10:24 - February 17, 2011
Habari ID: 2082258
Mashindano ya kitaifa ya qiraa ya Qur'ani Tukufu yamefanyika India katika mji mkuu wa Uttar Pradesh, Lucknow mnamo Februari 14.
Mashindano hayo ya Qur'ani yaliyoandaliwa na Madrasa ya Irfania yalikuwa na washiriki 25 kutoka majimbo kadhaa ya India kama vile Gujarat, Maharashtra, Bengal, Tamil Nadu, Bihar na jimbo mwenyeji Uttar Pradesh.
Mashindano hayo yalikamilika kwa kuzawadiwa maqari watatu ambao kwa mujibu wa rai ya jopo la majaji ndio waliokuwa wasomaji bora. Aidha walitunukiwa shahada za heshima na bodi ya utendaji ya mashindano hayo.
748898
captcha