IQNA

Kitabu cha Masomo ya Msingi ya Qur'ani chachapishwa

10:46 - February 17, 2011
Habari ID: 2082353
Kitabu cha Masomo ya Msingi ya Kiraa Sahihi ya Qur'ani kimechapishwa katika mji mtakatifu wa Qum chini ya usimamizi wa Kituo cha Qur'ani cha Hadhrat Ruqayyah (as).
Kitabu hicho kimeandikwa na Haidar al Kaabi, mhadhiri wa sayansi ya Qur'ani katika Kituo cha Hadhrat Ruqayyah na kina masomo saba ya jinsi ya kutamka maandishi na herufi za Qur'ani kwa njia sahihi, harakati za Qur'ani, alama za kusimama na kadhalika.
Kituo cha Hadhrat Ruqayyah pia kimetayarisha CD ya kiraa kamili ya Qur'ani iliyosomwa na Usadh Rafi A'amiri.
CD hiyo imetayarishwa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya kiraa na tartili ya Qur'ani kwa wanaopenda kushiriki masomo hayo. 749015


captcha