IQNA

Kikao cha Mashia na Masuni kufanyika Syria

14:05 - February 20, 2011
Habari ID: 2083701
Kikao cha 8 katika mfululizo wa warsha za Masuni na Mashia kitafanyika nchini Syria na kujadili “Changamoto za Ulimwengu wa Kiislamu”.
Hujjatul Islam Mujtaba Husseini mwakilishi wa Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Syria amesema kuwa, sambamba na Wiki ya Umoja baina ya Kiislamu, Maulamaa wa Kishia na Kisuni watakutana Damascus kujadili matatizo ya ulimwengu wa Kiislamu.
Ameongeza kuwa, “Kikao cha nane kitajadili upotofu na shaka kuhusu umoja wa Waislamu na washiriki watajaribu kuwasilisha mapendekezo ya kusuluhisha matatizo yaliyopo”.
Akiashiria warsha zilizotangulia, amesema kuwa, ‘njama za maadui za kuvuruga umoja wa Mashia na Masuni na njia za kukabiliana na njama hizo ni kati ya mambo yaliyojadiliwa katika vikao vilivyopita’.
749707
captcha