IQNA

Mpango wa Ujue Uislamu kutekelezwa Kanisa la Norwich Uingereza

20:09 - March 02, 2011
Habari ID: 2089487
Kanisa la Norwich la Uingereza lina mpango wa kutayarisha ratiba ya Ujue Uislamu kwa shabaha ya kuwaelimisha Wakristo dini ya Kiislamu na kutoa mtazamo mpya kuhusu majirani zao Waislamu.
Kituo cha habari cha networknorwich kimeripoti kuwa ratiba hiyo ya siku mbili inajumuisha hotuba mbalimbali za kuarifisha dini hiyo.
Maudhui kuu ya vikao vya ratiba hiyo ni jinsi ya kuujua Uislamu na kujenga uhusiano na jirani Waislamu.
Maudhui nyingine zitakazojadiliwa katika vikao hivyo ni pamoja na Uslamu wa zama hizi, Ujue Uislamu na jinsi ya kujenga uhusiano na jirani Waislamu. 756616

captcha