Kwa mujibu wa gazeti la Al Ra'y Abdullah Mahdi Barak amesema kikao hicho kinalenga kuchunguza nafasi ya Qur'ani katika sekta ya elimu.
Amesema kikao hicho kimeandaliwa na Taasisi ya Al Seraj al Munir chini ya kaulimbiu ya "kuelekea kwenye mafundisho bora ya Qur'ani".
"Kustawisha harakati za Qurani, kubainisha nafasi ya Qur'ani katika uga wa elimu, kustawisha utamaduni wa familia katika masuala ya elimu na mafundisho ya kidini na kubadilishana mawazo taasisi za kitaifa na kimataifa ni kati ya malengo ya kikao hicho", imesema taarifa ya Wizara ya Awqaf.
759234