IQNA

Chuo cha Uwekezaji wa Kiislamu kuanzishwa India

16:09 - March 07, 2011
Habari ID: 2091946
Chuo cha kuwafunza Waislamu kuhusu uwekezaji katika sekta mbalimbali za kifedha ikiwa ni pamoja na masoko ya hisa, mabenki n.k kwa mujibu wa misingi ya sheria za Kiislamu kitaanzishwa nchini India.
Chuo hicho kitaanzishwa na shirika la Wealth Management Pvt. Ltd lenye makao yake Mumbai India. Shirika hilo ambalo hutoa muongozo kuhusu kusimamia utajiri kwa mujibu wa sheria za Kiislamu limesema chuo hicho kinawahimiza vijana kujisajili katika kozi zake ili waweze kupata ajira na kufanya biashara katika sekta ya fedha yenye idadi ndogo ya Waislamu hivi sasa.
Mkurugenzi wa Pragmatic Wealth Management Pvt. Ltd Dkt. M Y Khan amesema kuna haja ya kuwepo na wataalamu Waislamu katika taasisi za kifedha na benki za Kiislamu.
759392


captcha