Katika maombolezo hayo filamu fupi ya maisha ya mwanazuoni huyo mashuhuri wa Kishia itaonyeshwa na pia waombolezaji kugawiwa cd za filamu hiyo ya kweli. Filamu hiyo inajumuisha maisha yake ya ujana akiwa masomoni na pia hotuba zake alizotoa katika vipindi tofauti vya maisha yake yenye mabaraka kubwa.
Ayatullah al-Amri aliaga dunia Jumatatu tarehe 24 Januari baada ya kuhudumia dini kwa miaka 60. Mazishi yake yalikuwa makubwa ambapo waombolezaji kutoka nchi tofauti za dunia walishiriki.
Shakhsia na viongozi tofauti wa Kiislamu walituma salama zao za rambirambi kufuatia kifo cha mwanazuoni huyo aliyepata mateso makubwa kutoka kwa utawala wa Kiwahhabi wa Saudi Arabia. 760209