IQNA

Jumuiya ya Kiislamu ya Uswisi yaanzishwa

16:59 - March 16, 2011
Habari ID: 2097111
Jumuiya ya Kiislamu ya Uswisi imeanzishwa kwa hima ya taasisi mbili za Kiislamu nchini humo.
Kituo cha habari cha journaldujura kimeripoti kuwa moja ya kazi muhimu za jumuiya hiyo ni kuanzisha majlisi itakayojumuisha wawakilishi wa Waislamu wote nchini humo.
Mwenyekiti wa Federesheni ya Jumuiya za Kiislamu nchini Uswisi (FOIS) Hisham Midhar amesema Waislamu wamekuwa barani Ulaya kwa miaka mingi sasa na kwamba lengo la kuasisiwa jumuiya hiyo ya Kiislamu ni kutaka itambuliwe kama taasisi ya kisheria ndani ya serikali ya Uswisi.
"Tunataka kuboresha sura ya Waislamu nchini Uswisi na taasisi hii mpya inapaswa kuwa chombo cha kuhuisha amani kati ya dini mbalimbali. "Tunataka kukomesha propaganda chafu za kuwaogopesha watu kuhusu dini ya Kiislamu", amesisitiza Hisham Midhar. 763912
captcha