IQNA

Maulamaa Indonesia wajadili matukio Mashariki ya Kati

14:13 - March 19, 2011
Habari ID: 2097502
Jumuiya ya Maulamaa wa Kiislamu ya Indonesia imefanya kikao cha kutathmini matukio yanayoendelea Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati.
Kikao hicho kilichunguza kwa makini matukio ya Afrika Kaskazini na Mashariki ya Kati kwa lengo la kuchukua maamuzi ya pamoja ya kukabiliana na changamoto zilizopo kwa maslahi ya Uislamu na Waislamu duniani.
Mabalozi wa nchi za Kiarabu na Kiislamu wameshirki katika kikao hicho na kati yao wakiwemo mabalozi au wawakilishi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Tunisia, Syria, Jordan, Sudan, Iraq n.k.
765034
captcha