Kwa mujibu wa gazeti la Ittihad linalochapishwa nchini Imarati, masomo hayo yaliyowashirikisha mahafidh 60 kutoka taasisi mbalimbali za Qur'ani na vituo vya kidini vya Imarati yalitoa mafunzo maalumu ya kuinua viwango vyao vya kielimu na hifdhi ya Qur'ani Tukufu. Kuwafahamisha washiriki thamani na sifa za jamii pamoja na kukidhiwa mahitaji yake na hasa yanayohusiana na masuala ya Qur'ani ni baadhi ya malengo ya kuandaliwa masomo hayo. 767238