IQNA

Waalimu 76,000 wa Qurani wafuzu Tehran

13:31 - April 03, 2011
Habari ID: 2099804
Waalimu 76,000 wa Qurani Tukufu wameshiriki na kufuzu katika kozi maalumu za mafundisho ya Qurani zilizofanyika katika mkoa wa Tehran nchini Iran kuanzia Macho 2010 hadi Machi 2011.
Kozi hizo zilitayarishwa na Taasisi ya Darul Quran ya Shirika la Kiislamu la Maendeleo kwa kushirikiana na vituo 318 vya Qurani kote Tehran.
Hayo yamedokezwa na Mahdi Nadi Mkuu wa Kituo cha Darul Quran mkoani Tehran. Ameongeza kuwa hivi sasa kuna kozi tano za waalimu wa shule za nursery ambapo waalimi 110 wa Tehran wanashiriki. Ameelezea matumaini kuwa kozi kama hizo zitaendelea katika siku za usoni.
764997
captcha