IQNA

Utawala wa Bahrain wachoma moto misikiti

16:51 - April 04, 2011
Habari ID: 2100525
Utawala wa Bahrain umechukua hatua hatari ya kuchochea hisia za kimadhehebu nchini humo kwa kuteketeza moto baadhi ya misikiti ya nchi hiyo kwa kisingizio kwamba ilijengwa bila vibali.
Misikiti mingi iliyochomwa moto inapatikana katika mtaa wa Hamad. Utawala huo pia umekuwa ukiwafuta kazi kiholela na kutowalipa mishahara watu walioshiriki katika maandamano ya hivi karibuni nchini humo wakitaka kufanyika marekebisho ya kisiasa katika muundo wa utawala huo. Wanafunzi na wanachuo walioshiriki katika maandamano hayo pia wamefukuzwa mashuleni na vyuoni. Wanazuoni wa Bahrain wanasema kuwa watawala wa nchi hiyo hata wamekuwa wakizuia watu waliojeruhiwa katika machafuko ya hivi karibuni kupata matibabu katika mahospitali ya nchi hiyo na kuwazuia madaktari kutoka nchi nyingine ambao wameomba kuingia nchini humo kwa lengo la kuwatibu majeruhi hao bila malipo. Utawala wa Manama umeanzisha wimbi kubwa la ukandamizaji dhidi ya Waislamu wa madhehebu ya Shia katika nchi hiyo na hata umekuwa ukiwatia mbaroni wanawake wajawazito na walio na umri mkubwa bila kujali lolote wala kuzingatia misingi ya utu katika kufanya hivyo. 768401
captcha