IQNA

Maonyesho ya bidhaa halali kufanyika China

17:09 - April 06, 2011
Habari ID: 2101794
Maonyesho ya Sita ya Kimataifa ya Chakula na Bidhaa Halali za Waislamu China (CHIHAS 2011) yatafanyika huko Yinchuan katika eneo lenye mamlaka ya ndani ya Ningxia Huo kuanzia Sept 19-23 yanatazamiwa kuwashirikisha zaidi ya wananuzi elfu 10 na washiriki 400.
Katika taarifa, Jumanne, kamati andalizi imesema maonyesho ya halali yalikuwa yamepangwa kuwa maonyesho ya kimataifa ya biashara kuonyesha bidhaa na huduma halali kwa mujibu wa mafundisho ya Kiislamu ili kuhudumia soko kubwa la kimataifa linalostawi.
'Kwa kuzingatia ongezeko la hitajio la bidhaa halali, Wizara ya Biashara ya China imeamua kuinua kiwango cha bidhaa halali'.
China inahesabiwa kuwa soko kubwa linaloibuka la bidhaa halali na ina soko la Waislamu milioni 150 nchini humo.
769827
captcha