Akizungumzia mashindano hayo Muhammad Sayyid Ba, Katibu Mkuu wa Shirika la Ustawi na Mafunzo ya Kiislamu la Senegal amesema kwamba Senegal imeteuliwa kuwa mwenyeji wa mashindano hayo kutokana na nafasi yake nzuri katika mafunzo ya Qur'ani. Amesema marefa wa mashindano hayo wamechaguliwa kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu. Mashindano hayo yanafanyika kwa mara ya kwanza barani Afrika. Mashindano hayo yanatazamiwa kumalizika hapo kesho Alkhamisi. 773594