IQNA

Semina ya 'Lulu ya Qur'ani' kufanyika Virginia Marekani

12:53 - April 14, 2011
Habari ID: 2105674
Semina ya Lulu ya Qur'ani imepangwa kufanyika katika mji wa Herndon katika jimbo la Virginia tokea tarehe 22 hadi 24 Aprili.
Kwa mujibu wa tovuti ya Almadina Institute' semina hiyo ya siku tatu itachunguza miujiza na mafundisho ya Qur'ani Tukufu. Wataalamu na wasomi wa Kiislamu kutoka nchi tofauti za Kiislamu watahudhuria kikao hicho na kuchunguza miujiza ya Qur'ani Tukufu pamoja na mafundisho muhimu yanayopatikana katikakitabu hicho kitakatifu. Kikao hicho kinaandaliwa na Jumuiya ya al-Madina kwa mwaka wa nne mfululizo. 773989
captcha